Ofisi ya haki za bindamu ya Umoja wa Mataifa, OHCHR imeelezea kusikitishwa na ongezeko la vitendo vya ghasia za kisiasa, ukatili dhidi ya wanawake na mashambulizi dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini Malawi, wakati huu uchaguzi ukitarajiwa kufanyika mwezi Mei mwaka huu wa 2019. Taarifa zaidi na Grace Kaneiya.