Ripoti mpya kuhusu matokeo ya utafiti wa kimataifa juu ya matumizi ya nishati kwa wanavijiji, iliotolewa wiki hii, na kuchapishwa bia na Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) pamoja na Idara ya Uingereza Inayohusika na Maendeleo Kimataifa (DFID) imethibitisha ya kuwa pindi uzalishaji wa japo kiwango kidogo cha nishati kutoka anuwai ya viumbehai utatekelezewa jamii za kienyeji, kadhia hiyo ina matumaini ya kuimarisha, kwa kiwango kikubwa, shughuli za maendeleo vijijini, hasa katika nchi masikini.