Jacques Diouf, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Chakula,na Kilimo (FAO) alitoa onyo maalumu hapo Ijumatano wakati alipokuwa anazuru Bara Hindi, ambapo alitahadharisha ya kuwa ulimwengu unawajibika kudhibiti kidharura hatari ya mifumko ya machafuko na vurugu, ambayo huenda ikachochewa na cheche mchanganyiko zinazotokana na kupanda kwa bei ya nishati kwenye soko la kimataifa, pamoja na ongezeko la mahitaji ya chakula duniani, na pia kuenea kwa tibuko la hali ya hewa ya kigeugeu katika ulimwengu, ikijumuika na matumizi ya kihorera ya ardhi ya kulimia kuzalisha nishati ya viumbe hai.