Mkutano wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mazingira ya binadamu, Stockholm+50, umeanza leo kwenye mji mkuu wa Sweden, Stockholm kwa wito kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizitaka nchi zote duniani kukumbatia haki za binadamu kwa ajili ya mazingira safi na yenye afya kwa wote hususan kwa jamii masikini, wanawake na wasichana, watu wa asili, vijana na vizazi vijavyo.