Dunia lazima ifanye jitihada zaidi ili kukomesha kuzorota kwa hali ya afya ya bahari, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo Jumapili, akiwataka vijana waliokusanyika Carcavelos, Ureno, kwa ajili ya jukwaa la vijana na ubunifu la Umoja wa Mataifa kuongeza kasi kwa sababu viongozi wa kizazi chake wanasuasua.