Zaidi ya watu milioni 50 wanatarajiwa kukabiliwa na viwango vya juu vya uhaba wa chakula (IPC Awamu ya 3 au zaidi*) mwaka huu 2022 katika nchi saba za IGAD (Djibouti, Ethiopia, Kenya, Somalia, Sudan Kusini, Sudan, Uganda) kwa mujibu wa toleo la mwaka 2022 la Mtazamo wa Kikanda wa IGAD kuhusu Majanga ya Chakula iliyotolewa leo.