Pembe ya Afrika inakabiliwa na hali ya ukame mkali zaidi kuwahi kurekodiwa tangu mwaka 1981, ambao unawaweka takriban watu milioni 13 kote Ethiopia, Kenya na Somalia katika hali ya kukabiliwa na njaa kali katika robo ya kwanza ya mwaka huu 2022, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP limeonya leo kupitia taarifa yake iliyotolewa jijini Nairobi, Kenya.