Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa, lile la chakula na kilimo, FAO na mpango wa chakula duniani, WFP yametoa ripoti inayotaja maeneo 20 duniani ambako janga la njaa linaweza kuchochewa na mizozo, mabadiliko ya tabianchi, COVID-19, madeni ya umma na vita ya Ukraine.