Mwakilishi wa shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF Nigeria, Peter Hawkins kupitia taarifa iliyotolewa hii leo katika mji mkuu wa Nigeria, Abuja, amesema amefarijika kupokea habari iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ya kuachiliwa kwa wanafunzi 27 wa Chuo cha Sayansi cha Serikali huko Kagara, ambao walitekwa nyara kutoka shule yao zaidi ya wiki moja iliyopita na kwamba anatarajia kurudi kwao salama katika familia zao.