Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema chanjo dhidi ya corona au COVID-19 ni muhimu ili kuhakikisha kila mtu kila mahali yuko salama dhidi ya janga hili hatari.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema katika kuwakumbuka waathirika milioni sita ambao ni Wayahudi na wengineo waliouawa kikatili wakati wa mauaji ya maangamizi makuu ya Holocust chini ya utawala wa Kinazi na washirika wao, inasikitrisha kwamba chuki dhidi ya Wayahudi bado inaendelea.
Historia ya kuvunja moyo imefikiwa duniani ambapo watu milioni 2 wamefariki dunia kutokana na ugonjwa utokanao na virusi vya Corona au COVID-19, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameelrezea huzuni yake kufuatia kifo cha afisa wa zamani wa ngazi ya juu kwenye umoja wa Mataifa Brian Urquhart aliyeutumikia Umoja wa Mataifa kwa miaka zaidi ya 40.
COVID-19 imebadili maisha yetu na kuutumbukiza ulimwengu katika mateso na huzuni. Ndivyo alivyoanza ujumbe wake wa mwaka mpya 2020, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, ujumbe alioutoa kwa njia ya video kutoka jijini New York, Marekani, makao makuu ya Umoja wa Mataifa.
Ikiwa leo ni siku ya wahamiaji duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesema ni mwaka wa kutathmini jinsi janga la Corona au COVID-19 lilivyosababisha mamilioni ya watu kukumbwa na machungu ya kutengana na familia zao na kutokuwa na uhakika wa ajira, jambo ambalo limewapatia watu hisia halisi ambazo wahamiaji hukumbana nazo kila wakati kwenye maisha yao.
Wakuu wa nchi na serikali mbalimbali 77 wameungana na viongozi wa makampuni ya biashara na kutana leo Jumamosi kwa njia ya mtandao kuzungumzia malengo na matamanio ya mabadiliko ya tabianchi na ahadi mpya za kuyatimiza.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya wafanyakazi wa kujitolea, Umoja wa Mataifa umetumia siku hii adhimu kuangazia wafanyakazi wa kujitolea na mchango wao katika kukabiliana na ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona au COVID-19.
Janga la ugonjwa wa Corona, COVID-19 likiendelea kutikisa duniani, Umoja wa Mataifa hii leo umeanza kikao maalum cha ngazi ya juu cha siku mbili kujadili janga hilo ambalo hadi sasa limesababisha vifo vya watu zaidi ya 1,400,000 duniani kote.
Mwaka huu azimio namba 1325 la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu wanawake na ulinzi na usalama duniani, limetimiza miaka 20 tangu kupitishwa kwake.