Wakati virusi vya Corona, COVID-19 vikiendelea kuibua sintofahamu duniani hivi sasa, shirika la utalii la Umoja wa Mataiaf, UNWTO limesema linashirikiana na shirika la afya ulimwenguni, WHO na wadau wengine kusaidia mataifa kutekeleza mikakati ya kupunguza rabsha zisizo za lazima katika safari na biashara za kimataifa.