Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, mamia ya wakimbizi kutoka Ukraine waliokimbilia Moldova, hasa wazee, familia zenye watoto wadogo na wanawake, wanapewa kipaumbele katika uhamisho wa kwenda nchi ya tatu, Romania kutoka Moldova kwa kuwa Moldova nchi iliyoko kwenye mpaka wa kusini mwa Ukraine ina rasilimali chache za kukabiliana na maelfu ya wakimbizi ambao wamevuka mpaka katika wiki za hivi karibuni.