Wakati leo ikiadhimishwa siku ya kimataifa ya utumaji fedha kwa familia , Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa ombi kwa watu kila mahali kuwaunga mkono wahamiaji katika wakati huu ambapo fedha ambazo zinatumwa nyumbani kwa familia na wahamiaji hao zimepungua kwa zaidi ya dola bilioni 100 na kusababisha njaa, kushindwa kusoma, na kuzorota kwa afya kwa mamilioni ya familia duniani.