Jumamosi ya leo, Shirika la afya ulimwenguni limethibitisha kupitia ofisi yake ya kanda ya ulaya kuwa virusi vya Corona au 2019-nCoV ambavyo kwa majuma kadhaa sasa vimesababisha madhara makubwa nchini China, sasa vimethibitika nchini Ufaransa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia hivi sasa iko katika hali ya taharuki na sintofahamu ikikabiliwa na mambo makubwa manne ambayo yanatishia mustakbali wa mamilioni ya watu na sayari yenyewe.
Kuna aina mbalimbali za sigara za kielektroniki kwa kiingereza Electronic Nicotine Delivery Systems au (ENDS), zikiwa na kiwango mbalimbali cha kichangamsho aina ya Nicotine na moshi hatarishi.
Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa,FAO litaimarisha uwezo wa mfumo wake wa ufuatiliaji wa misitu ulimwenguni na hii ni kutokana na ushirikiano wake mpya na shirika la anga za juu la Japan, JAXA.
Pengo la usawa duniani linaongezeka kwa zaidi ya asilimia 70 ya watu wote duniani na hivyo kuongeza hatari ya migawanyiko na kuathiri maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Lakini ongezeko hilo linaweza kudhibitiwa na kushughulikiwa katika ngazi ya kitaifa na kimataifa kwa mujibu wa ripoti ya utafiti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo Jumanne.
Takribani nusu ya watu bilioni moja wanafanya kazi saa chache za kulipwa kuliko zile ambazo wangependa au kukosekana kabisa kwa kazi za kulipwa. Hiyo ni kwa mujibu wa riupoti mpya ya shirika la kazi duniani.
Ripoti ya shirika la fedha duniani IMF iliyotolewa leo kuhusu hali ya ukuaji wa uchumi duniani katika robo ya kwanza inaonyesha kwamba uchumi wa dunia bado unasuasua ingawa ni wenye utulivu baada ya kushuka kwa miaka miwli mfululizo.
Katika kuelekea maiak 75 ya Umoja wa Mataifa itakayoadhimishwa baadaye mwaka huu , Baraza la Usalama la Umoja huo limeahidi dhamira yake ya kudumisha katiba ya Umoja wa Mataifa ambayo ndio nguzi ya kuanzishwa kwa Umoja huo na pia kwa utulivu wa kimataifa kwa msingi wa sheria za kimataifa.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Australia limetuma salamu zake za masikitiko kwa watoto na familia zilizoathirika na janga la moto linaloendelea kote nchini Australia.