Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Afya ya Mimea, IDPH, ulimwengu ukiadhimisha siku hiyo kwa mara ya kwanza, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, limesema mabadiliko ya tabianchi na shughuli za binadamu zinabadilisha mifumo ikolojia na kuharibu bayonuai huku hali hiyo ikiunda maeneo mapya kwa ajili ya wadudu waharibifu kustawi.