Shirika la Umoja wa Mataifa la kufanikisha upatikanaji wa dawa za tiba kwa gharama nafuu, UNITAID, leo limetangaza makubaliano ya kuwezesha dawa ya kutibu ugonjwa wa Corona, COVID-19 kutoka kampuni ya Pfizer ipatikane kwa gharama nafuu kwa nchi za kipato cha chini na kati.