Bila mnepo wa uchumi wa nchi za ukanda wa Asia Mashariki na Pasifiki, kusingalikuwepo na kuibuka kwa biashara duniani mwishoni mwa mwaka uliopita wa 2020, wamesema wachambuzi wa biashara kutoka wa Umoja wa Mataifa wakati wakiwasilisha hii leo ripoti ya mwelekeo wa biashara duniani.