Ripoti ya utafiti mpya iliyotolewa leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Madawa na Uhalifu UNODC imesema, wahamiaji ambao wanatumia mitandao ya usafirishaji haramu kukimbia nchi zao mara nyingi wanakabiliwa na ukatili wa kupindukia, mateso, ubakaji na kutekwa wakiwa njiani au wanaokoshikiliwa mateka.