COVID-19 imebadili maisha yetu na kuutumbukiza ulimwengu katika mateso na huzuni. Ndivyo alivyoanza ujumbe wake wa mwaka mpya 2020, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, ujumbe alioutoa kwa njia ya video kutoka jijini New York, Marekani, makao makuu ya Umoja wa Mataifa.
Ikiwa leo ni siku ya wahamiaji duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesema ni mwaka wa kutathmini jinsi janga la Corona au COVID-19 lilivyosababisha mamilioni ya watu kukumbwa na machungu ya kutengana na familia zao na kutokuwa na uhakika wa ajira, jambo ambalo limewapatia watu hisia halisi ambazo wahamiaji hukumbana nazo kila wakati kwenye maisha yao.
Wakuu wa nchi na serikali mbalimbali 77 wameungana na viongozi wa makampuni ya biashara na kutana leo Jumamosi kwa njia ya mtandao kuzungumzia malengo na matamanio ya mabadiliko ya tabianchi na ahadi mpya za kuyatimiza.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya wafanyakazi wa kujitolea, Umoja wa Mataifa umetumia siku hii adhimu kuangazia wafanyakazi wa kujitolea na mchango wao katika kukabiliana na ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona au COVID-19.
Janga la ugonjwa wa Corona, COVID-19 likiendelea kutikisa duniani, Umoja wa Mataifa hii leo umeanza kikao maalum cha ngazi ya juu cha siku mbili kujadili janga hilo ambalo hadi sasa limesababisha vifo vya watu zaidi ya 1,400,000 duniani kote.
Mwaka huu azimio namba 1325 la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu wanawake na ulinzi na usalama duniani, limetimiza miaka 20 tangu kupitishwa kwake.
Hatimaye mkataba wa kimataifa wa kupinga matumizi ya silaha za nyuklia, TPNW, utaanza kutumika tarehe 22 mwezi Januari mwaka ujao wa 2021 baada ya Honduras kuwa mwanachama wa 50 wa Umoja wa Mataifa kuridhia mkataba huo jana jumamosi, hatua ambayo imeelezewa kuwa zama mpya ya kutokomeza silaha za nyuklia duniani.
Leo ni siku ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni maadhimisho ya miaka 75 tangu kuanzishwa kwa chombo hicho mwaka 1945 huko San Francisco nchini Marekani wakati huu wanachama waanzilishi wakiwa ni 50.
Kamati ya tuzo ya amani ya Nobel yenye makao yake nchini Norway leo imelitangaza shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP kuwa ndio mshini wa tuzo ya amani ya Nobel kwa mwaka huuu wa 2020.
Hatimaye mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umefunga rasmi pazia lake hii leo na kuashiria kuanza kwa mkutano wa 75 wa Baraza hilo, ambalo ni moja vyombo vikuu vya Umoja wa Mataifa wenye wanachama 193.