Ukosefu wa usawa, suala ambalo linaainisha zama zetu za sasa, linahatarisha kusambaratisha chumi za dunia na jamii hivi sasa, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres katika hotuba yake aliyoitoa jijini New York, Marekani hii leo katika kuadhimisha Mhadhara wa Nelson Mandela kwa mwaka 2020.