Shirika la afya ulimwenguni, WHO limetoa mwongozo na mbinu za kuwezesha viongozi kwenye maeneo ya majiji kuweza kukabiliana na visababishi vikuu vya vifo kwenye maeneo hayo.
Zaidi ya nusu ya idadi ya watu duniani hivi sasa wanaishi mijini na kufikia mwaka 2050 theluthi mbili ya watu watakuwa wanaishi mjini na makazi ya kuendana na ongezeko la watu bado hayajakarabatiwa na miji mipya itahitaji kujengwa.
Utafiti mpya wa shirika la afya ulimwenguni, WHO, umebaini kuwa theluthi mbili ya wanawake wenye uwezo wa kubeba mimba na ambao wana nia ya kuchelewesha kupata ujauzito au kudhibiti idadi ya watoto huacha kutumia huduma za uzazi wa mpango kwa hofu ya madhara ya huduma hizo.
Amani, usalama, upendo na mshikamano ndio msingi wa mustakabali wa dunia, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku ya Umoja wa Mataifa hii leo.
Ripoti mpya ya shirika la afya duniani, WHO, imesema kuwa watu wengi zaidi walipata tiba dhidi ya ugonjwa wa Kifua Kikuu, TB, mwaka 2018 kuliko wakati wowote ule kutokana na kuimarika kwa mbinu za utambuzi wa ugonjwa huo.
Ikiwa leo ni siku ya chakula duniani wito ukiwa ni kutokomeza njaa- na kuwa na dunia ambako chakula chenye lishe bora kinapatikana kwa bei nafuu na kwa watu wote na kila mahali, Umoja wa Mataifa unahoji iweje leo hii zaidi ya watu milioni 820 hawana chakula cha kutosheleza mahitaji yao.
Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa saratani, IARC na wadau wake wamezindua toleo la tatu la atlasi au kitabu cha ramani kinachoonesha hali ya saratani duniani.
Idadi kubwa ya watoto wanateseka kutokana na lishe duni na mifumo ya chakula ambayo inawadumaza, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF katika ripoti kuhusu hali ya watoto duniani kwa mwaka huu wa 2019 ikiangazia zaidi watoto, chakula na lishe.
Katika kuelekea siku ya chakula duniani ambayo kila mwaka hufanyika Oktoba 16, shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO, limesema kila mwaka theluthi moja ya chakula kinachozalishwa kwa ajili ya matumizi ya binadamu kina pote bure au kutupwa. Maelezo zaidi na Flora Nducha