Mishahara midogo, mazingira duni ya kazi kwa katika vyombo vya uvuvi, ufugaji wa samaki na miundo mbinu mibovu ya viwanda vya usindikaji ni vina athari kubwa katika maisha ya kila siku ya wafanyakazi.
Ikiwa leo ni miaka 100 tangu kuzaliwa Sir. Brian Urquhart, mmoja wa wafanyakazi waanzilishi zaidi wa Umoja wa Mataifa, Katibu Mkuu Antonio Guterres ameumwagia sifa lukuki ikiwemo utumishi uliotukuka na uliosaidia kujenga misingi ya chombo hicho kilichoundw mwaka 1945 baada ya Vita Vikuu vya Pili vya dunia.
Kukomesha ukoloni kumesaidia kubadili uanachama wa Umoja wa Mataifa na kupanua wigo wa wanachama kutoka 51 wa awali na kufikia 193 hivi leo. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza hii leo katika ufunguzi wa mkutano wa kamani maalumu ya Umoja wa Mataifa ya kutokomeza ukoloni mjini New York Marekani.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limesema mwaka jana 2018 mahitaji ya kuwapatia wakimbizi nchi ya tatu ya hifadhi yalikuwa ni chini ya asilimia 5 licha ya kwamba mwaka huo ulivunja rekodi ya idadi ya kubwa ya wakimbizi waliosaka hifadhi ya nchi ya tatu.
Mbali ya kuburudisha , kuelimisha na kuleta kipato kwa maelfu ya watu wanaoikumbatia, sanaa pia ni chachu ya kuchagiza amani kwakuwa inawaleta watu pamoja, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amepokea taarifa rasmi ya utekelezaji wa makubaliano ya Prespa ambayo yanafanya kufikiwa muafaka wa kuanza kutumika kwa jina la Jamhuri ya Marcedonia Kaskazini, taarifa ya msemaji wa Katibu Mkuu imeeleza.
Takwimu za Shirika la afya ulimwenguni, WHO zinaonyesha kuwa idadi ya maambukizi ya surua inaongezeka katika maeneo mabli mbali na sio changamoto ya bara moja
Ikiwa leo ni siku ya radio duniani , kauli mbiu ikiwa majadiliano, uvumilivu na amani, mkoani Kagera nchini Tanzania wananchi nao wamepaza sauti kuhusu umuhimu wa njia hiyo adhimu ya mawasiliano na kile ambacho kinapaswa kufanyika ili kuhakikisha taarifa kutoka chombo hicho zina mantiki.
Vijana zaidi ya bilioni moja wa umri wa kati ya miaka 12 na 35 wanajiweka katika hatari ya kupata uziwi usioweza kutibika kwa sababu ya kusikiliza sauti za juu za vitu kama muziki kwa kutumia simu za kisasa za rununu zinazoweza kufanya mambo mengi.
Wanasayansi, watunga sera , wawakilishi wa serikali , wakulima na walaji wanakutana kwa siku mbili mjini Adis Abba Ethiopia kwenye mkutano wa kwanza kuhusu uhakika na usalama wa chakula na jukumu lake katika maendeleo endelevu, SDG’s.