Ikiwa kesho Aprili 14 ni siku ya ugonjwa wa Chagas, shirika la kimataifa la kufanikisha uwepo wa tiba nafuu duniani, Unitaid linaloratibiwa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, limesema uwepo wa Covid-19 umefanya hali kuwa mbaya zaidi kwa hali ambayo tayari ilikuwa mbaya kutokana na ugonjwa wa Chagas.