Mashirika ya Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira duniani UNEP, na la chakula na kilimo FAO yamesema mimea ndio kila kitu katika kuhakikisha uhai wa mamilioni ya watu duniani na sayari tunayoishi, lakini cha kusikitisha ni kwamba mara nyingi mimea hiyo haipewi uzito unaostahili.