Licha ya kupunguzwa kwa bajeti na kuongezeka kwa majeruhi na vifo miongoni mwa walinda amani, bado ulinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa unabakia kuwa nyenzo muhimu katika kuchagiza amani na utulivu duniani, amesema mkuu wa operesheni za ulinzi wa aman iza Umoja wa Mataifa.