Watu bilioni 1.3 katika nchi 109 duniani ni maskini wa kila hali na kiwango cha umaskini huo kinatofautiana kikabila, kwa kundi au rangi, hiyo ni kwa mujibu wa uchambuzi mpya kuhusu kiwango cha umaskini wa kila hali duniani ikiwemo kiafya, kielimu na kiwango cha maisha, uliotolewa leo na Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.