Virusi aina ya Omnicron vikiendelea kuwa sababu ya kasi kubwa ya maambukizi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19 hivi sasa duniani kote, shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO hii leo limesema ni muhimu hatua zaidi zikachukuliwa ili kusaidia nchi zote kupata haraka iwezekanavyo chanjo dhidi ya Corona kwa kuwa ndio mkombozi iwapo mtu anaambukizwa na tayari ana chanjo.