Wakati duniani inasubiri kwa hamu chanjo dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICF, nalo limeanza maandalizi ya kuhakikisha chanjo hiyo inatolewa na kusambazwa mapema na kwa usalama kwa kununua na kuhifadhi mabomba ya sindano na vifaa vingine vya kufanikisha zoezi hilo.