Umoja wa Mataifa ukitimiza miaka 75, wakazi wa sayari ya dunia kutoka nchi maskini hadi tajiri, wanawake hadi wanaume, vijana hadi watoto wametoa maoni yao kuhusu Umoja wa Mataifa wautakao, ikiwa ni matokeo ya utafiti uliofanyika kuanzia mwezi Januari mwaka huu kufuatia wito wa Katibu Mkuu Antonio Guterres.