Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema maono ya baba wa taifa la India, Mahatma Gandhi yameendelea kuvuma ulimwenguni kote kupitia kazi za umoja huo za maelewano, usawa, maendeleo endelevu, uwezeshaji vijana na suluhu ya amani ya mizozo.