Huku kukiwa na joto kali, ukame na moto wa nyika, sehemu nyingi za dunia zilikuwa zimepitia mojawapo ya Julai tatu zenye joto zaidi katika rekodi, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la hali ya hewa WMO hii leo.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO hii leo limetangaza bei za vyakula zilishuka kwa kiasi kikubwa mwezi Julai,2022 na kuashiria kushuka kwa mwezi wa nne mfululizo tangu zilipoweka rekodi ya juu zaidi mwanzoni mwa mwaka kufuatia vita ya Ukraine.
Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA, leo limetaja washindi 10 wa pamoja wa shindano la miradi bunifu inayoweza kuleta mabadiliko chanya na kuwezesha wanawake na wasichana duniani.
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO, limesema nchi zinapaswa kushirikiana kukomesha haraka kuenea kwa ugonjwa wa ndui ya nyani, au Monkeypox bila kujali utaifa, rangi ya mtu au dini, amesema afisa mwandamizi wa shirika hilo hii leo.
Wakati zaidi ya robo tatu ya watu wazima wote wanaoishi na Virusi vya UKIMWI VVU wanapata aina fulani ya matibabu, idadi ya watoto wanaofanya hivyo, inafikia asilimia 52 pekee.
Hatimaye meli ya kwanza yenye shehena ya tani elf 26 za mahindi imeondoka leo katika bandari ya Odesa nchini Ukraine ikielekea Tripoli nchini Lebanon ikiwa ni kuanza utekelezaji wa makubaliano yaliyosainiwa tarehe 22 Julai mwaka huu baina ya Urusi na Ukraine chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa.
Umoja wa Mataifa una wasiwasi mkubwa kuhusu kukosekana kwa matarajio ya kuanza tena kwa juhudi za kidiplomasia za kumaliza vita nchini Ukraine. Amesema leo Mkuu wa Idara ya siasa kwenye Umoja wa Mataifa Rosemary DiCarlo, akizungumza katika Baraza la Usalama jijini New York Marekani.
Huku kukiwa na kura 161 za ndio, na nchi nane hazikupiga kura, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha hii leo azimio la kutambua upatikanaji wa mazingira safi, yenye afya na endelevu kama haki ya binadamu kwa wote.
Leo dunia inaadhimisha siku ya Homa ya ini ulimwenguni, ambayo imewekwa kwa lengo la kujenga uelewa kwa jamii juu ya ugonjwa huu unaoshambulia ini kwa kasi na kushindwa kufanya kazi yake vizuri.
Umoja wa Mataifa tarehe 11 mwezi Julai 2022 ilitangaza kwamba idadi ya watu duniani inatarajiwa kufikia bilioni 8 mnamo tarehe 15 Novemba 2022 ikiwa ni hatua muhimu kwa ubinadamu na ikaenda mbali zaidi kutangaza kuwa mwaka 2023 India inakadiriwa kuwa nchi yenye watu wengi zaidi, kuipita China.