Tarehe 8 Oktoba, sauti ya makofi makubwa na yasiyo ya kawaida ilisikika karibu na chumba cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa huko Geneva, Uswisi. Vita vilivyopiganwa kwa miongo kadhaa na wanaharakati wa mazingira na watetezi wa haki, mwishowe vilizaa matunda.