Mabadiliko ya mwelekeo yanayolinganisha sekta binafsi na malengo ya kimataifa yahahitajika ili kushughulikia changamoto za siku za usoni, pamoja na zile zilizosababishwa na janga la corona au COVID-19, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa hii leo Jumatatu, akihutubia kongamano la Ufadhili kwa ajili ya Maendeleo (FfD).