Ikiwa leo ni siku ya maji duniani , Katibu Mkuu wa Umoja wa Mastaifa Antonio Guterres amesema upatikanaji wa maji ni kinga dhidi ya maradhi,utu na changamoto zinazotokana na mabadiliko ya tabianchi na hasa panapokuwa na mzunguko unaosimamiwa vizuri wa maji ukijumuisha maji ya kunywa, usafi wa mazingira na kujisafi, maji taka, na mambo menghine muhimu.