UNESCO, kupitia taarifa yake iliyotolewa hii leo mjini Paris Ufaransa, inahimiza uangalifu mkubwa baada ya kupokea ripoti nyingi za udanganyifu na usafirishaji haramu wa mali za kitamaduni za Kiafrika kwa kutumia nyaraka za uongo zikidai kuwa UNESCO inathibitisha biashara kama hiyo na hata kuthibitisha thamani ya bidhaa hizo.