Mkuu ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia misaada ya dharura, OCHA, Mark Lowcock hii leo mjini New York Marekani ametangaza kuwa zimetolewa dola za kimarekani milioni 25 kutoka kwenye mfuko wa dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF, kusaidia mashirika yanayoongozwa na wanawake ambayo yanapambana dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia.