Leo ni siku ya kimataifa ya Yoga ambayo ni maadhimisho ya sita ya Umoja wa Mataifa yanayofanyika kila mwaka Juni 21, kwa lengo la kutambua aina ya zamani ya mazoezi haya kama njia ya kuboresha afya na ustawi, lakini pia kama nyenzo yenye uwezo wa kukabiliana na changamoto na msongo uliosababishwa na janga la virusi vya corona au COVID-19.