Migogoro mingi ya kimataifa inasababisha kuzorota kwa hali ya soko la ajira duniani, na kuongezeka kwa ukosefu wa usawa ndani ya nchi na kati ya nchi na nchi. Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi Duniani, (ILO).