Ingawa binadamu anadhurika kwa kiasi kikubwa na madhara ya mabadiliko ya tabianchi bado serikali haziwezi mifumo ya kutosha kulinda afya za wananchi wao, limesema shirika la afya ulimwenguni, WHO katika ripoti ya tathmini yake ya kwanza kabisa iliyotolewa hii leo ikimulika nchi 101.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumza katika vikao mbalimbali mwanzoni mwa mkutano wa 25 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP25 hii leo huko Madrid Hispania na kusisitiza hatua thabiti na mshikamano katika kutekeleza makubaliano ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Umoja wa Mataifa umesema jamii ikiwa ni pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali, asasi za kiraia na wanaharakati wana mchango mkubwa katika vita dhidi ya UKIMWI.
Ikiwa leo ni siku ya televisheni duniani, shirika la mawasiliano la Umoja wa Mataifa, ITU limesema chombo hicho cha mawasiliano kitaendelea kuwa na umuhimu mkubwa katika kuongeza uelewa wa masuala ya mambo miongoni mwa binadamu.
Kuelekea maadhimisho ya miaka 75 ya Umoja wa Mataifa mwakani 2020, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo ametangaza kuwa maadhimisho hayo yatajumuisha mjadala jumuishi wa dhima ya jukumu la ushirikiano wa kimataifa katika kujenga mustakabali utakiwao ulimwenguni.
Amani, usalama, upendo na mshikamano ndio msingi wa mustakabali wa dunia, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku ya Umoja wa Mataifa hii leo.
Ikiwa leo ni siku ya chakula duniani wito ukiwa ni kutokomeza njaa- na kuwa na dunia ambako chakula chenye lishe bora kinapatikana kwa bei nafuu na kwa watu wote na kila mahali, Umoja wa Mataifa unahoji iweje leo hii zaidi ya watu milioni 820 hawana chakula cha kutosheleza mahitaji yao.
Baada ya mkutano wa ngazi ya juu kuhusu hatua kwa tabianchi uliotanguliwa na harakati za vijana kutaka hatua, Katibu Mkuu wa Umoja Mataifa Antonio Guterres aliweka tafakuri yake kwenye tahariri iliyochapishwa na ubia wa vyombo vya habari 170 wenye wasomaji zaidi ya mamilioni.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo ameziandikia barua nchi wanachama kuhusu ukata mbaya zaidi kuwahi kukabili chombo hicho chenye wanachama 193 kwa karibu muongo mmoja.