Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa, HLPF, limeendelea likiangazia masuala kadhaa ikiwemo maadhimisho ya miaka 25 tangu kufanyika kwa mkutano wa kimataifa wa idadi ya watu na maendeleo, ICPD, huko mjini Cairo nchini Misri.