Leo ni siku ya kimataifa ya kumbukizi na kutambua waathirika na manusura wa vitendo vya ugaidi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumza kwenye tukio maalum lililofanyika katika makao makuu ya chombo hicho jijini New York, Marekani akisema kuwa ugaidi na aina zake zote umesalia changamoto kubwa.
Leo ni siku ya huduma za kibinadamu duniani ambapo Umoja wa Mataifa unapigia chepuo mwaka huu wanawake waliojikita katika kutoa huduma za kibinadamu kote ulimwenguni.
Kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani hii leo Naibu Katibu Mkuu wa chombo hicho Amina J. Mohammed ameongoza tukio la maadhimisho ya siku ya watu wa asili, ambayo maudhui yalikuwa lugha za asili.