Mikataba ya Geneva juu ya Hifadhi ya maisha na hishima ya wanadamu wasioshiriki kwenye mapigano - hususan, raia, wafanyakazi wa afya, wahudumia misaada ya kiutu, pamoja na wagonjwa, wanajeshi majeruhi na mateka wa vita - imetimia miaka 60 mnamo tarehe ya leo, 12 Agosti 2009. KM ameeleza kwenye taarifa aliotoa juu ya kumbukumbu hiyo kwamba kanuni ya Mikataba ya Geneva zimefanikiwa "kudumishwa na kuvumiliwa na umma wa ulimwengu kwa muda mrefu" kwa sababu ya umuhimu unaopewa sheria hizo na jumuiya ya kimataifa. KM alipendekeza kwa Mataifa Wanachama yote kuchukua hatua zinazofaa, kuhakikisha kanuni za kimsingi za Mikataba ya Geneva huwa zinatekelezwa na wote kama ipasavyo.