Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na idadi ya watu na afya ya uzazi duniani UNFPA, hii leo limezindua ombi maalum la dola milioni 835 likiwa ni ombi lake kubwa zaidi la kibinadamu ili liweze kuwafikia zaidi ya wanawake, wasichana na vijana milioni 54 katika nchi 61 mwakani 2022 kwa ajili ya kutoa msaada muhimu.