Baada ya kuhitimisha ziara yake katika maeneo yaliyoathiriwa, Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mratibu wa Misaada ya Kibinadamu nchini Ufilipino, Gustavo Gonzalez, leo Desemba 23 amesema Kimbunga Rai "kimekuwa cha uharibifu," na kubainisha kuwa katika siku zijazo, idadi ya majeruhi na waliofariki "bila shaka" itaongezeka.