Wakati picha kamili ya mwaka 2020 bado haijafahamika, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, linakadiria kuwa uhamishaji wa kulazimishwa ulimwenguni au ufurushwaji ulizidi milioni 80 katikati ya mwaka, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi kuhusu mwenendo wa uhamishaji wa kulazimishwa ulimwenguni.