Mahakakama ya uhalifu wa kivita nchini Cambodia ambayo inaungwa mkono na Umoja wa Mataifa imekamilisha kusikiliza rufani ya watuhumiwa wa uhalifu uliofanywa wakati wa kiongozi wa zamani wa taifa hilo Khmer Rouge.
Mionzi ya nyuklia inayoendelea kuvuja kwenye mtambo wa Fukushima Daiichi nchini Japan umewafanya maelfu ya raia wa nchi hiyo kusalia na wasiwasi wa afya zao.
Gharama kubwa za chakula zimezuia watu milioni 19.4 katika nchi za Asia -Pacific kujikwamua na umasikini mwaka jana imesema ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon kwa ushirikiano na mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Ukimwi UNAIDS Michel Sidibe leo wamezindua rasmi ripoti ya Ukimwi mjini Nairobi Kenya.
Mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu madeni ya nje na haki za binadamu Cephas Lumina amepongeza mfumo wa maendeleo wa Vietnam ambao unamuweka raia wa nchi hiyo kuwa kitovu cha maendeleo ya taifa.