Wiki ya biashara mtandao inayosimamiwa na Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Biashara na Maendeleo, UNCTAD ikiwa imeanza, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed amesema wiki hiyo inatoa fursa ya kuangalia upya matumizi ya data na mifumo na majukwaa ya kidijitali kwa ajili ya maendeleo endelevu.