Dktr Margaret Chan, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Afya Duniani (WHO) kwenye mahojiano na waandishi wa habari mwisho wa wiki [25/04/2009], alihadharisha mripuko wa karibuni wa aina ya virusi vya homa ya mafua - inayotambuliwa kwa umaarufu kama homa ya mafua ya nguruwe - katika maeneo ya Mexico na Marekani, inatakikana kudhibitiwa mapema, au si hivyo homa hii inaashiriwa itaenea kwa kasi na kudhuru fungu kubwa la umma wa kimataifa.