António Guterres, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) Alkhamisi alianza ziara rasmi ya siku tatu katika Pakistan, kufanya tathmini ya mahitaji ya dharura ya kihali ya raia 800,000 waliong\'olewa makazi, kutokana na mapigano makali yalioshtadi karibuni baina ya vikosi vya Serikali na wapambanaji wapinzani, kwenye eneo la kaskazini-magharibi.