Dktr Margaret Chan, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la WHO, kwenye mashauriano ya kiwango cha juu kuhusu maambukizi ya homa ya mafua ya A(H1N1) yaliofanyika Geneva Ijumatatu, alitilia mkazo umuhimu wa kuripoti "taarifa halisi za kitaaluma, zinazoaminika, juu ya vipengele mbalimbali vilivyodhihiri kuhusu ugonjwa huu, na kuwawezesha wataalamu kufanya maamuzi ya dharura ya kudhibiti bora mfumko wa maradhi kwa kujitayarisha kukabiliana na janga hilo kimataifa."